Vikembe
- Vikembe pia huitwa vizawa.
- Vikembe ni wana wa viumbe mbalimbali.
Mifano;
- Malaika - Mtoto wa binadamu.

- Ndama - Mtoto wa ng’ombe, ndovu.


- Funutu/maige/kimatu/tunutu - Mtoto wa nzige.

- Jana/chana – Mtoto wa nyuki.

- Kifaranga – Mtoto wa kuku.

- Kinda – mtoto wa ndege/nyuni.



- Kiluwiluwi – Mtoto wa chura, mbu.

- Kiwavi – Mtoto wa kipepeo.

- Kitungulekituju – Mtoto wa sungura.

- Kihongwe – Mtoto wa punda.

- King’onyo – Mtoto wa mdudu.

- Kilebu – Mtoto wa mbwa/kelbu.

- Kigunge - mtoto wa nyami.

- Kivinimbi – Mtoto wa nguruwe.

- Chengo – Mtoto wa nyangumi.

- Kinyaunyau – Mtoto wa paka.

- Kibuli/kimeme – Mtoto wa mbuzi.

- Nyumbu – Mtoto kati ya punda na farasi.

- Chotara/hafukasti/suriama/shombe – mtoto kati ya wazazi wa rangi mbalimbali.
- Saraka/athiari/jarari/dawati – mtoto wa meza.
- Kimatu/maige/tunutu/matumatu/funutu - mtoto wa nzige.
- Kitekli - mtoto wa farasi.

- Kigwena - mtoto wa mamba.

- Kikuto'kisui/chongole - mtoto wa fisi.

- Nirigi/nirihi - mtoto wa ngamia.

- Kidanga - mtoto wa ndovu.

- Nyamawa - mtoto wa mbweha.

- Kibebe/katama - mtoto wa kondoo.

- Kichengo - mtoto wa samaki.

- Kinyemere - mtoto wa nyoka.